Friday, May 12, 2017

Rais Sudani Kusini amfuta kazi mkuu wa majeshi

Juba.

Habari zinasema kuwa, Rais Salva Kiir, amechukua hatua ya kumfuta kazi Paul Malong Awan, kufuatia majenerali wengi wa ngazi ya juu jeshini kujiuzulu kutokana na kuwepo ubaguzi na jinai nyingi za kivita zinazofanywa na jeshi la Sudan Kusini.

Rais Salva Kiir akimpandisha cheo mkuu mpya wa Majeshi
James Ajongo

 Habari zinasema kuwa, Rais Kiir amemteua James Ajongo kuchukua nafasi ya Malong Awan kwa ajili ya kusimamia shughuli za jeshi la taifa hilo changa zaidi barani Afrika. Inafaa kuashiria kuwa, mbali na serikali ya Juba kupambana na wanamgambo wa upinzani, lakini pia jeshi la serikali nalo linakabiliwa na mgogoro wa ndani, ambapo makamanda kadhaa jeshini wamekuwa wakitangaza kujiuzulu nyadhifa zao.

Sudan Kusini ilitumbukia katika machafuko mwezi Disemba mwaka 2013, baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa makamu wake Riek Machar kwamba alikula njama za kutaka kumpindua. Katika machafuko hayo, maelfu ya watu wameuawa na mamilioni ya wengine kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi.

Licha ya kufikiwa makubaliano ya usitishaji vita mwezi Agosti mwaka 2015, lakini bado machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe vinaendelea nchini Sudan Kusini.

Trump alaumiwa kwa mapokezi aliyompa Lavrov

Serikali ya Marekani imekumbwa na changamoto mpya kufuatia kuenea picha za Rais Donald Trump wa nchi hiyo akimkaribisha kwa hadhi Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov katika ikulu ya White House.

Rais Trump akizungumza na Waziri wa Mambo ya nje wa
Urusi Sergey Lavrov(kushoto) Ikulu mjini Washington.

Rais Trump amekutana na Lavrov pamoja na balozi wa Russia mjini Washington, Sergueï Kisliak katika ikulu ya nchi hiyo. Hata hivyo, picha zilizomuonyesha Trump akionyesha tabasamu kwa kukutana na viongozi hao wa Russia, zimeibua malalamiko kwa Wamarekani ambao wanaiona Moscow kuwa hasimu wa taifa hilo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Marekani, mkutano huo wa Trump na viongozi hao wa Russia, haukuwafurahisha wanadiplomasia wa Marekani na kwamba mapokezi ya Trump kwa Lavrov hufanyiwa viongozi wenye hadhi ya urais. Habari zaidi zinasema kuwa, kitendo cha kutandikwa zulia jekundu kwa wanadiplomasia hao wa Russia, ni harakati ya kuzisifia siasa za Moscow, katika hali ambayo hadi sasa nchi hiyo inatuhumiwa kuingilia uchaguzi wa rais wa mwaka jana nchini Marekani.

Wamarekani anaoandamana kumpinga Rais Trump
Katika mkutano huo baina ya Rais Donald Trump na Sergey Lavrov viongozi hao wamezungumzia juu ya namna ya kutekelezwa makubaliano kwa ajili ya kutengwa maeneo yenye kiwango cha chini cha mivutano chini Syria hususan karibu na mipaka ya Syria na Jordan. Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, katika mazungumzo hayo hakukujadiliwa vikwazo vya Marekani na nchi za Ulaya dhidi ya nchi yake.

Wednesday, February 15, 2017

Rais Hassan Rouhani wa Iran azitembelea Kuwait na Oman

Kuwait City.

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Amir wa Kuwait wamesisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano wa nchi jirani na za Kiislamu hasa kwa kuzingatia hali ya hivi sasa Mashariki ya Kati.

Rsis Hassan Rouhani akizungumza na Emir wa Kuwait
Sheikh Sabah Al- Ahmad Al-Jaber Al-Sabah

Rais Hassan Rouhani wa Iran na Amir wa Kuwait Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah wamesisitiza hayo katika mkutano wao mjini Kuwait Jumatano usiku. Akiwa katika  ziara rasmi nchini Kuwait, Rais wa Iran amemfahamisha Amir wa nchi hiyo kuwa nchi mbili hizi zina nukta za pamoja za kiutamaduni, kihistoria na kidini na kwamba uhusiano wa karibu na wa kidugu wa nchi mbili umekuwepo kwa muda mrefu.
Rais Rouhani amesema kuna fursa nyingi za kuimarisha uhusiano wa Iran na Kuwait katika nyanja mbali mbali.


Aidha amesema hivi sasa eneo la Mashariki ya Kati linakabiliwa na hatari kubwa ya ugaidi na kuongeza kuwa, tatizo hilo ambalo linawasibu wote linaweza kutatuliwa kwa ushirikiano wa nchi za eneo. Rais Rouhani amesisitiza haja ya nchi za eneo kujiepusha na mifarakano na kuongeza kuwa, 'sote tunapaswa kuishi kwa pamoja kwa msingi wa udugu wa Uislamu na tujiepushe na mifarakano.


Kwa upande wake, Amir wa Kuwait Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah amesema amefurahishwa na safari ya Rais wa Iran nchini Kuwait pamoja na mitazamo yake ya kuleta umoja. Amir wa Kuwait amesema kwa kuzingatia hali ya sasa katika eneo, nchi yake ina azma ya kuimarisha uhusiano wa pande zote na Iran. Sheikh Al Sabah amesisitiza ulazima wa umoja na mashikamano wa nchi za eneo na Waislamu kwa ujumla kutokana na hali ya hivi sasa katika eneo na kuongeza kuwa: "Sisi sote ni Waislamu na kwa kuzingatia udugu wetu tunapaswa kuishi kwa pamoja katika mkondo wa ustawi, uthabiti na amani."


Rais wa Iran pia mapema Jumatano alitembelea Oman na kufanya mazungumzo na Sultan Qaboos wa nchi hiyo.
Baada ya safari yake hiyo ya siku moja nchini Kuwait na Oman, Rais Rouhani alirejea Tehran jana usiku.

Waziri wa mambo ya nje wa Oman aikosoa Saudi Arabia kwa kupendelea vita


Muscat.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Yusuf bin Alawi ameikosoa Saudi Arabia kutokana na kushupalia utumiaji njia za kijeshi badala ya diplomasia kwa ajili ya kutatua migogoro ya eneo la Mashariki ya Kati.

Waziri wa mambo ya nje wa Oman bwana Yusuph bin Alawi
Akizungumza katika mahojiano aliyofanyiwa na kanali ya televisheni ya Kiarabu ya Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC, Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman ameashiria kushupalia Saudia utumiaji njia za kijeshi kwa ajili ya kutatua migogoro ya eneo na kueleza kwamba: Badala ya njia za kjeshi, matatizo na migogoro ya eneo inapasa itatuliwe kwa njia za kidiplomasia.

Akizungumzia safari aliyofanya nchini Syria, Bin Alawi ametetea hatua yake hiyo kwa kueleza kwamba: Syria ni nchi ya Kiarabu na Oman haijavunja uhusiano wake wa kidiplomasia na nchi hiyo.


Kuhusu upatanishi wa nchi yake kwa ajili ya kutatua mgogoro wa Yemen, Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman amesema, kitu kinachopewa umuhimu na Oman ni kusimamishwa vita na kutatuliwa hitilafu zilizopo kulingana na matakwa ya wananchi wa Oman.

Yusuf bin Alawi amesisitizia pia nchi za eneo hili kupambana na ugaidi na kueleza kwamba magaidi wakiwemo wa Daesh wamehatarisha amani na uthabiti wa eneo

Saturday, December 10, 2016

MELI YENYE MAROLI 600 MALI YA DANGOTE CEMENT YATIA NANGA BANDARI YA MTWARA.

Mfanyabiashara tajiri zaidi barani Afrika, Alhaji Aliko Dangote leo December 10, alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Dk Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam. Dangote alimthibitishia rais Magufuli kuwa hana lengo la kufunga kiwanda chake kama inavyodaiwa badala yake anatafuta fursa nyingine za kuwekeza hapa nchini.


Katika kuthibitisha hilo, Mfanyabiashara huyo alisema leo meli yenye malori mapya 600 kwa ajili ya kusambazia saruji yake itawasili nchini. Ameongeza kuwa lengo la kufanyabiashara hapa nchini mbali na kutengeneza faida pia ana lengo la kuisaidia serikali ya Tanzania kutengeneza ajira hivyo hana sababu ya kuagiza mali ghafi toka nje ya nchi ambazo zinapatikana hapa nchini.

Mara tu baada ya kumaliza mazungumzo na Rais, Meli kubwa yenye baadhi ya magari hayo imetia nanga katika bandari ya Mtwara ambapo ndipo kiwanda cha Saruji cha Dangote kilipo. Pia imeelezwa kuwa wiki ijayo meli nyingine kutoka Korea Kusini yenye malori 451 inatarajiwa kuwasili katika bandari ya Mtwara.

Pichani ni  meli hiyo ikiwa bandarini Mtwara




DR. MAGUFULI NA ALHAJI DANGOTE WAFANYA MAZUNGUMZO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Dar es salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Desemba 2016, amekutana na kufanya mazungumzo na Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara, Alhaji Aliko Dangote.

Rais John Magufuli na Mmiliki wa kiwanda cha
Dangote Cement, Alhaji Aliko Dangote wakifanya mazungumzo
Ikulu Jijini Dar es salaam leo December 10, 2016.


Katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amemhakikishia mfanyabiashara huyo kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wote nchini katika kutimiza lengo lake la kuwa na Tanzania ya Viwanda.

Rais Magufuli amesema kuhusu kiwanda cha kuzalisha Saruji cha Dangote kilichopo Mkoani Mtwara hapakuwa na tatizo lolote ila kulikuwa na watu ambao walitaka kujinufaisha binafsi kupitia mradi huo kwa kufanya biashara za ujanja kitu ambacho serikali yake haikiruhusu.
Amemtaka Dangote kununua gesi moja kwa moja kutoka TPDC ambacho ni chombo cha serikali badala ya kutumia watu ambao wamekuwa na nia ya kutengeneza faida tu.


''Iwapo unataka maelezo yoyote ama lolote linalokukwamisha uwasiliane na viongozi wa serikali badala ya kuwasiliana na watu ambao wako kwa ajili ya kufanya biashara ya ujanja ujanja kwa lengo la kupiga dili '' amesema Rais Magufuli.
Dokta Magufuli amesema Dangote ametaka eneo dogo ambalo angelitumia kusafirishia saruji yake wakajitokeza watu ambao wametaka kumuuzia kwa shilingi bilioni 43 kitu ambacho hakina uhalisia wowote bali ni watu ambao wanataka kutengeneza faida kitu ambacho hakiwezekani.

Kwa upande wake mmiliki wa Kiwanda cha kuzalisha Saruji cha Dangote, Alhaji Aliko Dangote ameshangazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa amefunga kiwanda kwa sababu amekatazwa kuagiza makaa ya mawe toka nje ya Tanzania kitu ambacho amesema hakiingii akilini kwa sababu makaa ya mawe ya Tanzania ni rahisi na yana ubora kuliko kuagiza nje.


Katika kuthibitisha hilo, tayari Mfanyabiashara huyo ameingiza malori mapya 600 kwa ajili ya kusambazia saruji yake. Ameongeza kuwa lengo la kufanya biashara hapa nchini mbali na kutengeneza faida pia ana lengo la kuisaidia serikali ya Tanzania kutengeneza ajira hivyo hana sababu ya kuagiza mali ghafi toka nje ya nchi ambazo zinapatikana nchini.

Rais Magufuli na Alhaji Dangote wakiongea na
waandishi wa habari mara baada ya kufanya mazungumzo
Ikulu jijini Dar es salaam.
Alhaji Dangote amemuhakikishia Rais magufuli kuwa ataendelea kufanya kazi na Serikali ya Tanzania na kamwe hana nia yoyote ya kufunga kiwanda chake kama inavyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari bali ana mpango wa kuangalia fursa nyingine zaidi za uwekezaji hapa nchini kutokana na uwepo wa sera nzuri za uwekezaji chini ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Saturday, November 12, 2016

MRADI WA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI

Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi. Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MTADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.
Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.


Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.
Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.
Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.
- paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
-mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
- layer's consetraite
Kilo 25 kifuko. = 21500.
Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.
Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.

Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.
TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake
Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.
Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500
-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga
Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.
Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.
Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe. Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.

Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote